Thursday, July 4, 2019

SABABU KWANINI BADO HAJAKWAMBIA MUOANE


1 Ni mwangalifu sana kwenye Viapo / ahadi zake. Baadhi ya wanaume wanaogopa sana kula viapo mana wanaogopa jambo hilo linaweza kuwa pigo kwao. Inaweza ikawa ni kwasababu alishakuwa na historia mbaya kuhusiana na mapenzi, labda mpenzi wake alimfanyia mambo ambayo siyo na akamgeuka, au vitisho vingine vinavyohusiana na hivyo vinaweza kuwa vimemtisha.
Haya mambo ya kujiwekea nadhiri yanaweza kusuluhika/ kushughulikiwa. Japo, itamgarimu muda sana kwa hilo wazo la kuoana kumuingia akilini, hivyo atakuwa anahitaji muda wa kulifikiria hilo swala kwa kina.
#2 Anawasiwasi kwamba ataukosa uhuru wake aliouzoea. Kwake, kuoana inaweza kuashiria kuongezeka kwa majukumu, tena hasa pale mnapoanza kuwa na watoto. Boyfriend wako anaweza akawa anajiuliza kuwa – ni vitu gani atavikosa akishakuweka ndani, na kutokana na hivyo vitu ni bora abaki bachelor au akuoe?
#3 Labda bado anampenda sana mpenzi wake wa zamani.
Mara nyingi, hii haitokei sana, lakini kama boyfriend wako hakuombi muoane, inawezekana bado anamkumbuka mpenzi wake wa zamani. Kama bado ana Like picha zake na luandika comments nzuri katika picha zake za Instagram, au kuongea na e mara nyingi, hizo zinaweza kuwa ishara za hatari

No comments:

Post a Comment